Skip to main content

Mr Ttouch aeleza siri ya kutengeza beats za nyimbo nyingi zinazofanya vizuri

Hakuna anayebisha kwamba kwa sasa producer wa ‘Touchez Sound’ Mr Ttouch kuwa ndiye producer anayefanya ngoma nyingi za hivi karibuni ambazo zinafanya vizuri.
Mtayarishaji huyo ambaye mpaka sasa ana ngoma kama Komela ya Dayna Nyange, Mazoea ya Billnass, Kibabe ya Professor J, Nisaidie Kushare ya Jay Moe na ngingine nyingi ambazo zinafanya vizuri, ameiambia Bongo5 siri ya kutengeneza beat kali.
“Nashukuru Mungu kama mashabiki wameshaanza kusema ninafanya vizuri, hicho ni kitu kizuri sana ambacho kila producer anakitaka,” alisema Mr Ttouch. “Kusema kweli siri ya mafanikio yangu ni kufanya kazi kwa bidii, pia watu wajue mimi siyo msikilizaji wa muziki huu wa kisasa, mimi nyimbo zangu zote nazikiliza nyimbo za zamani, ni nyimbo ambazo zinanipa mambo mengi sana,”
Aliongeza,”Mimi nasikiliza ngoma alizo-producer Master J kipindi cha nyuma, P-Funk Majani na maproducer wengine wengi wa zamani. Nikizikiliza kuna vitu fulani ambavyo navipana na vinaweza kunisaidia kuboresha kazi zangu ndio maana kila beat nikifanya watu wanasema ni kali,”




WEKA COMMENT YAKO HAPO CHINI

Comments

Popular posts from this blog

PICHA ZA MUONEKANO WA GARI LA SIMBA SPORT CLUB

Basi la klabu ya Simba SC aina ya Yutong sasa lina muonekano mpya baada ya  wadhamini wazamani TBL kupitia Kilimanjaro kumaliza mkataba wao na timu hiyo. Mwonekano wake safari hii, kuna picha za wachezaji mbalimbali.

MCHEZAJI WA NICE YA UFARANSA AMESEMA ALIKUA MWATHIRIKA WA UBAGUZI WA RANGI

Mchezajiwa wa klabu ya Nice ya nchini Ufaransa Mario Balotelli anasema kuwa alikuwa mwathiriwa wa ubaguzi wa rangi wakati wa mechi ya Ijumaa dhidi ya Bastia. Balotelli ambaye mchezaji hyo wa zamani wa Liverpool mwenye umri wa mika 26 aliandika katika mtandao wa kijamii akisema, ni jambo la kawaida kwamba wafuasi wa Bastia hufanya makelele ya tumbili kwa mechi yote na hakuna mtu katika idara ya adhabu anayechukua hatua? ”Kwa hivyo ubaguzi wa rangi ni sheria halali nchini Ufaransa? Ama ni Bastia pekee? Soka ni mchezo mzuri lakini watu kama wafuasi wa Bastia wanaharibu.Ni aibu kubwa”. Balotelli ambaye alicheza dakika 90 aliporudi uwanjani baada ya kutumikia adhabu yake ya mechi waliyo toka sare ya 1-1 huko Corsica. Ujumbe huo uliotumwa katika mtandao wa Instagram ulisambazwa na Nice katika mtandao wa Twitter wa klabu hiyo. Jopo la adhabu la ligi ya Ufaransa ambalo hutoa maamuzi halijatoa tamko lolote. Balotelli amesha funga mabao 10 katika mechi 15 tangu alivyo jiunga na ...

MARIO BALOTELLI BADO ANDELEZA VITUKO VYAKE

Mchezaji mtukutu Mario Balotelli bado anaendelea na vituko vyake baada ya  kupata kadi nyekundu na kutolewa nje ya dimba kwenye dakika za majeruhi wakati timu yake ya Nice ilipotoka suluhu ya 0-0 na Bordeaux. Hii ilikuwa ni katika mtanange wa Ligi Kuu ya Ufaransa maarufu kama Ligue 1. Sare hiyo ya bila kufungana inaifanya klabu hiyo ya Nice kuzidi kukaribiwa point na klabu ya soka ya Monaco kwenye msimamo wa ligi hiyo ambapo sasa inaongoza kwa tofauti ya alama 2 pekee. Mshambuliaji huyo wa zamani wa Liverpool na Manchester City alipatiwa kadi nyekundu ya moja kwa moja baada ya kumfanyia rafu mbaya Lewczuk ambaye ni beki.