Skip to main content

Huu ni ufafanuzi kutoka Mahakama ya Tanzania kuhusu uteuzi wa Kaimu Jaji Mkuu

Mahakama ya Tanzania imewathibitishia wananchi kuwa itaendelea kufanya kazi zake kwa mujibu wa Katiba na Sheria na kwa jitihada kubwa bila woga, hofu, huba wala chuki kwa wadau wote kama inavyopaswa.
Taarifa iliyotolewa Dar es Salaam kwa vyombo vya habari na Jaji Kiongozi, Ferdinand Wambali ilieza pia kwamba hakuna kosa la kikatiba lililofanywa na Rais John Magufuli kwa kumteua Kaimu Jaji Mkuu kama inavyopotoshwa na baadhi ya vyombo vya habari.
Rais Magufuli Januari 17, mwaka huu alimteua Profesa Ibrahim Juma kuwa Kaimu Jaji Mkuu wa Tanzania kuchukua nafasi iliyoachwa wazi na Jaji Mkuu mstaafu, Mohamed Othman. Jaji Kiongozi alikuwa anatoa ufafanuzi wa habari iliyochapishwa katika gazeti moja la kila wiki, mwanzoni mwa wiki hii ikiwa na kichwa cha habari ‘Utata Jaji Mkuu.’
Alifafanua katika taarifa yake kwamba kichwa cha habari kilichoelezwa kwenye gazeti hilo kinatoa taswira hasi dhidi ya utendaji wa Mahakama na mchakato wa kupata Jaji Mkuu.
Akizungumzia uteuzi wa Kaimu Jaji Mkuu, Jaji Wambali alisema; “Kwanza ni vizuri ikaeleweka kuwa Mamlaka ya uteuzi inayo mamlaka chini ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano waTanzania ya 1977 kufanya uteuzi wa Kaimu Jaji Mkuu kama ilivyofanya kwa kuzingatia mazingira makuu matatu kama yalivyoelezwa kwenye Ibara ya 118 (4) (a), (b) na (c) ya Katiba.
“Hakuna shaka kuwa mazingira yaliyopelekea kuteuliwa kwa Kaimu Jaji Mkuu tarehe 17/1/2017 na kuapishwa tarehe 18/1/2017 ni kutokana na kiti cha Jaji Mkuu kuwa wazi kama ilivyoelezwa katika Ibara ya 118(4) (a) ya Katiba baada ya aliyekuwapo Mheshimiwa Jaji Mkuu Mohamed Chande Othman kustaafu baada ya kufikia umri uliowekwa kwa mujibu wa Katiba.
“Kwa msingi huo mamlaka ya uteuzi ambayo ni Rais imetekeleza wajibu wake wa awali kwa kuzingatia matakwa ya Katiba kama ilivvoelezwa katika Ibara ya 118(4) (c) kuhusu sifa za aliyeteuliwa kuwa miongoni mwa Majaji wa Mahakama ya Rufani.
“Kwa mujibu wa Katiba pia Kaimu Jaji Mkuu anapaswa kufanya kazi hiyo hadi atakapo teuliwa Jaji Mkuu kama inavyoelezwa katika Ibara ya 118 (5).”
Jaji Wambali alisema kutokana na matakwa hayo ya kikatiba, hakuna uvunjaji wowote wa Katiba kama baadhi ya watu wanavyodhani.
Alisema pia ni vizuri ikaeleweka kuwa Jaji anapoteuliwa kuwa Kaimu Jaji Mkuu anapaswa kutekeleza majukumu yote ya ofisi ya Jaji Mkuu kama yalivyoainishwa kwenye Katiba, Sheria na Kanuni mbalimbali.
“Vile vile anapaswa kufanya hivyo kwa kujiamini bila hofu kama anavyopaswa kufanya kazi ya ujaji. “Kwa msingi huo kazi za utoaji haki katika mhimili wa Mahakama ambao kwa sasa uko chini ya uongozi wa Kaimu Jaji Mkuu zinaendelea kutekelezwa nchini kama zinavyotakiwa kwa kuzingatia Katiba na sheria kupitia kwa Majaji, Mahakimu na watumishi wengine bila hofu, upandeleo au chuki kama ambavyo kiapo cha wote wanaohusika kinavyotaka,” alisema Jaji Wambali.
Aidha, alisema hakuna sababu yoyote ya wananchi na wadau wote wa Mahakama kuhofu kuwa yapo mambo ambayo yamekwama, yameyumba au yatayumba katika kipindi kinaposubiriwa uteuzi wa Jaji Mkuu.
SOCIAL MEDIA CAMPAIGN FOLLOW ME NA SHARE 
ANGALIAVIDEO MBALIMBALI KUPITIA YOUTUBE YANGU JONGO ABDALLAH

Comments

Popular posts from this blog

PICHA ZA MUONEKANO WA GARI LA SIMBA SPORT CLUB

Basi la klabu ya Simba SC aina ya Yutong sasa lina muonekano mpya baada ya  wadhamini wazamani TBL kupitia Kilimanjaro kumaliza mkataba wao na timu hiyo. Mwonekano wake safari hii, kuna picha za wachezaji mbalimbali.

MCHEZAJI WA NICE YA UFARANSA AMESEMA ALIKUA MWATHIRIKA WA UBAGUZI WA RANGI

Mchezajiwa wa klabu ya Nice ya nchini Ufaransa Mario Balotelli anasema kuwa alikuwa mwathiriwa wa ubaguzi wa rangi wakati wa mechi ya Ijumaa dhidi ya Bastia. Balotelli ambaye mchezaji hyo wa zamani wa Liverpool mwenye umri wa mika 26 aliandika katika mtandao wa kijamii akisema, ni jambo la kawaida kwamba wafuasi wa Bastia hufanya makelele ya tumbili kwa mechi yote na hakuna mtu katika idara ya adhabu anayechukua hatua? ”Kwa hivyo ubaguzi wa rangi ni sheria halali nchini Ufaransa? Ama ni Bastia pekee? Soka ni mchezo mzuri lakini watu kama wafuasi wa Bastia wanaharibu.Ni aibu kubwa”. Balotelli ambaye alicheza dakika 90 aliporudi uwanjani baada ya kutumikia adhabu yake ya mechi waliyo toka sare ya 1-1 huko Corsica. Ujumbe huo uliotumwa katika mtandao wa Instagram ulisambazwa na Nice katika mtandao wa Twitter wa klabu hiyo. Jopo la adhabu la ligi ya Ufaransa ambalo hutoa maamuzi halijatoa tamko lolote. Balotelli amesha funga mabao 10 katika mechi 15 tangu alivyo jiunga na ...

MARIO BALOTELLI BADO ANDELEZA VITUKO VYAKE

Mchezaji mtukutu Mario Balotelli bado anaendelea na vituko vyake baada ya  kupata kadi nyekundu na kutolewa nje ya dimba kwenye dakika za majeruhi wakati timu yake ya Nice ilipotoka suluhu ya 0-0 na Bordeaux. Hii ilikuwa ni katika mtanange wa Ligi Kuu ya Ufaransa maarufu kama Ligue 1. Sare hiyo ya bila kufungana inaifanya klabu hiyo ya Nice kuzidi kukaribiwa point na klabu ya soka ya Monaco kwenye msimamo wa ligi hiyo ambapo sasa inaongoza kwa tofauti ya alama 2 pekee. Mshambuliaji huyo wa zamani wa Liverpool na Manchester City alipatiwa kadi nyekundu ya moja kwa moja baada ya kumfanyia rafu mbaya Lewczuk ambaye ni beki.