Skip to main content


Kipindi cha The Weekend Chat Show cha Clouds TV sasa kutaitwa SHILAWADU. Mabadiliko ya kipindi hicho cha burudani yataenda sambamba na ujio wa Shilawadu Ubuyu Tour ambapo watangaji wa kipichi hicho, mastaa pamoja mashabiki watapata fursa ya kupanda basi hilo la tour na kukutana na mastaa wao huku kipindi kikirekodiwa.

Qwhisar Thomson mmoja kati ya watangazaji wa kipindi hicho
Akizungumza na waandishi wiki hii mmoja kati ya watangazaji wa kipindi hicho, Qwhisar Thomson alisema kipindi hicho kimeenda mtaani ili kutoa shukrani kwa mashabiki pamoja na kuwapa fursa ya kukutana na mastaa ambao wamekuwa wakihojiwa kila siku.
“Kwanza tunawashukuru mashabiki wetu, mastaa pamoja na wadau mbalimbali kwa kuwa pamoja na sisi kuanzia mwanzo mpaka sasa hivi,” alisema Qwhisar “Lakini katika namna ya kuwashukuru zaidi tunaenda mtaani na tour basi yetu kuwapa fursa mashabiki ya kukutana na mastaa wao pamoja na kuwauliza yale ambayo wamekuwa wakiyauliza kupitia mitandao ya kijamii.,”
Qwhisar alisema tuor ya Shilawadu Ubuyu Tour itaanza Desemba 24 kwa wakazi wa wilaya ya Temeke, baada ya hapo itaingia Kinondoni pamoja na Ilala.
Pia kipindi hicho kimetambulisha bidhaa yake mpya ya ubuyu wenye jina la kipindi chao ‘SHILAWADU’.

Comments

Popular posts from this blog

PICHA ZA MUONEKANO WA GARI LA SIMBA SPORT CLUB

Basi la klabu ya Simba SC aina ya Yutong sasa lina muonekano mpya baada ya  wadhamini wazamani TBL kupitia Kilimanjaro kumaliza mkataba wao na timu hiyo. Mwonekano wake safari hii, kuna picha za wachezaji mbalimbali.

MCHEZAJI WA NICE YA UFARANSA AMESEMA ALIKUA MWATHIRIKA WA UBAGUZI WA RANGI

Mchezajiwa wa klabu ya Nice ya nchini Ufaransa Mario Balotelli anasema kuwa alikuwa mwathiriwa wa ubaguzi wa rangi wakati wa mechi ya Ijumaa dhidi ya Bastia. Balotelli ambaye mchezaji hyo wa zamani wa Liverpool mwenye umri wa mika 26 aliandika katika mtandao wa kijamii akisema, ni jambo la kawaida kwamba wafuasi wa Bastia hufanya makelele ya tumbili kwa mechi yote na hakuna mtu katika idara ya adhabu anayechukua hatua? ”Kwa hivyo ubaguzi wa rangi ni sheria halali nchini Ufaransa? Ama ni Bastia pekee? Soka ni mchezo mzuri lakini watu kama wafuasi wa Bastia wanaharibu.Ni aibu kubwa”. Balotelli ambaye alicheza dakika 90 aliporudi uwanjani baada ya kutumikia adhabu yake ya mechi waliyo toka sare ya 1-1 huko Corsica. Ujumbe huo uliotumwa katika mtandao wa Instagram ulisambazwa na Nice katika mtandao wa Twitter wa klabu hiyo. Jopo la adhabu la ligi ya Ufaransa ambalo hutoa maamuzi halijatoa tamko lolote. Balotelli amesha funga mabao 10 katika mechi 15 tangu alivyo jiunga na ...

MARIO BALOTELLI BADO ANDELEZA VITUKO VYAKE

Mchezaji mtukutu Mario Balotelli bado anaendelea na vituko vyake baada ya  kupata kadi nyekundu na kutolewa nje ya dimba kwenye dakika za majeruhi wakati timu yake ya Nice ilipotoka suluhu ya 0-0 na Bordeaux. Hii ilikuwa ni katika mtanange wa Ligi Kuu ya Ufaransa maarufu kama Ligue 1. Sare hiyo ya bila kufungana inaifanya klabu hiyo ya Nice kuzidi kukaribiwa point na klabu ya soka ya Monaco kwenye msimamo wa ligi hiyo ambapo sasa inaongoza kwa tofauti ya alama 2 pekee. Mshambuliaji huyo wa zamani wa Liverpool na Manchester City alipatiwa kadi nyekundu ya moja kwa moja baada ya kumfanyia rafu mbaya Lewczuk ambaye ni beki.