Skip to main content

SIMU ZENTE GHARAMA KUBWA DUNIANI MWAKA 2016

Simu za Smartphones zimekuwa ni kati ya vitu vinakimbizana na teknolijia kila kukicha, na ni moja kati ya vifaa ambavyo vimekuwa seheme ya maisha ya karibu asilimia 70 ya watu duniani lote, kuna wakati simu tunazomiliki zimekuwa zinatoa majibu ya wewe ni mtu wa aina gani.
Simu zimekuwa zikitengenezwa kuleta ushindani wa teknolojia lakini kupima uwezo wa kifedha wa watumiaji na mapenzi.
Kwa mujibu wa The Merkle wamezitaja aina 5 za simu ambazo mpaka kufikia mwezi December 2016 zimekuwa ni simu zilizovunja rekodi ya kuuzwa kwa bei ya juu kuliko simu nyingine zozote duniani. Japokuwa hizi simu ni za kawaida ila tu zimekuwa zikiongezewa urembo wa madini ya thamani kubwa ili kuzipa muonekano wa kipekee .
5.- GOLDVISH LE MILLION ($1.3 MILLION) (Zaidi ya Tsh. Bilioni 2.8)
Sifa ya hii simu ukiishika kama sio mmliki wake inapiga kelele zenye sauti ya kuonesha imeibiwa. Cover la nje lote limeunda kwa Almasi ya Karat 120, na cover la ndani limeundwa kwa dhahabu ya kutosha.
4.- DIAMOND CRYPTO SMARTPHONE ($1.3 MILLION) (Zaidi ya Tsh. Bilioni 2.8)
Diamond-Crypto-Smartphone
Simu hii imeundwa na mtaalmu wa madini aitwaye Peter Aloisson na ilitoka kwa mara ya kwanza mwaka 2006, Simu hii ya Diamond Crypto Smartphone iliundwa kwasababu maalumu za kutunza siri, kwa mujibu wa watengenezaji wake. Simu hii hutumia OS ya Windows CE kama mfumo mkuu wa uendeshaji wake.  Simu hii imeundwa kwa madini ya Almasi ambapo kuna vipande 50 pia vya Almasi ya blue.
3.- AMOSU CALL OF DIAMOND IPHONE 6 ($3 MILLION) (Zaidi ya Tsh. Bilioni 6.5)
Alexander Amosu ndiye mtengenezaji wa simu hii ambaye mwanzo alikuwa akifanya biashara ya kuuza ringtone za simu. Kwasasa anaziongezea urembo simu na kuziuza kwa mastaa wa muziki, wacheza filamu, wanamichezo pamoja na watu maarufu wenye uwezo mkubwa kifedha.
The Call of Diamond ni simu aina ya iPhone 6 ambayo imenakshiwa kwa Gold ya Karat 18 kwenye cover lake la ndani wakati kwa nje imewekewa vipande vya Almasi vinavyofikia 6,127 na inamaliziwa na logo ya Cupertino moja ya makampuni makubwa duniani. 
2.- BLACK DIAMOND IPHONE 5 ($15 MILLION) (Zaidi ya Tsh. Bilioni 32.6)
Kama ulidhani dola milioni 3 ni nyingi kununua simu sasa kutana na hii, inaitwa Black Diamond iPhone 5. Simu hii imeundwa kwa Gold inayifikia Karat 26, Almasi iliyotiwa rangi nyeusi pia imeongeza urembo kwenye simu hii. Black Diamond inatengenezwa na kampuni ya mfanyabiashara kutoka China  anaitwa Stuart Hughes.
1.- FALCON SUPERNOVA IPHONE 6 ($100 MILLION) (Zaidi ya Tsh. Bilioni 217.8)Most Expensive iPhone 6
Bila shaka umeona gap lililopo kutoka simu iliyoshika nafasi ya pili! Hii ni iPhone 6s ambayo kila kitu kilichopo kwenye simu hii ni madini ya Almasi, Gold pamoja na Ruby. Mzigo unaitwa The SuperNova pamoja na bei hiyo bado unaambiwa hii sio simu ya gharama kati ya zilizowahi kuundwa.

Comments

Popular posts from this blog

PICHA ZA MUONEKANO WA GARI LA SIMBA SPORT CLUB

Basi la klabu ya Simba SC aina ya Yutong sasa lina muonekano mpya baada ya  wadhamini wazamani TBL kupitia Kilimanjaro kumaliza mkataba wao na timu hiyo. Mwonekano wake safari hii, kuna picha za wachezaji mbalimbali.

MCHEZAJI WA NICE YA UFARANSA AMESEMA ALIKUA MWATHIRIKA WA UBAGUZI WA RANGI

Mchezajiwa wa klabu ya Nice ya nchini Ufaransa Mario Balotelli anasema kuwa alikuwa mwathiriwa wa ubaguzi wa rangi wakati wa mechi ya Ijumaa dhidi ya Bastia. Balotelli ambaye mchezaji hyo wa zamani wa Liverpool mwenye umri wa mika 26 aliandika katika mtandao wa kijamii akisema, ni jambo la kawaida kwamba wafuasi wa Bastia hufanya makelele ya tumbili kwa mechi yote na hakuna mtu katika idara ya adhabu anayechukua hatua? ”Kwa hivyo ubaguzi wa rangi ni sheria halali nchini Ufaransa? Ama ni Bastia pekee? Soka ni mchezo mzuri lakini watu kama wafuasi wa Bastia wanaharibu.Ni aibu kubwa”. Balotelli ambaye alicheza dakika 90 aliporudi uwanjani baada ya kutumikia adhabu yake ya mechi waliyo toka sare ya 1-1 huko Corsica. Ujumbe huo uliotumwa katika mtandao wa Instagram ulisambazwa na Nice katika mtandao wa Twitter wa klabu hiyo. Jopo la adhabu la ligi ya Ufaransa ambalo hutoa maamuzi halijatoa tamko lolote. Balotelli amesha funga mabao 10 katika mechi 15 tangu alivyo jiunga na ...

MARIO BALOTELLI BADO ANDELEZA VITUKO VYAKE

Mchezaji mtukutu Mario Balotelli bado anaendelea na vituko vyake baada ya  kupata kadi nyekundu na kutolewa nje ya dimba kwenye dakika za majeruhi wakati timu yake ya Nice ilipotoka suluhu ya 0-0 na Bordeaux. Hii ilikuwa ni katika mtanange wa Ligi Kuu ya Ufaransa maarufu kama Ligue 1. Sare hiyo ya bila kufungana inaifanya klabu hiyo ya Nice kuzidi kukaribiwa point na klabu ya soka ya Monaco kwenye msimamo wa ligi hiyo ambapo sasa inaongoza kwa tofauti ya alama 2 pekee. Mshambuliaji huyo wa zamani wa Liverpool na Manchester City alipatiwa kadi nyekundu ya moja kwa moja baada ya kumfanyia rafu mbaya Lewczuk ambaye ni beki.