Skip to main content

Bonucci: Napenda tukutane na Barcelona, Bayern ni hatari zaidi

Mchezaji wa klabu ya Juventus Leonardo Bonucci amefunguka kuwa angependa kukutana na Barcelona kwenye mechi za robo fainali ligi ya Mabingwa msimu huu.
Juventus wamefanikiwa kutinga robo fainali baada ya kuitoa Porto kwenye michuano hiyo, na Bonucci anatamani droo ya Ijumaa iwakutanishe na Barca ili walipize kisasi cha 2014-15 dhidi ya timu hiyo.
“Klabu yetu ni miongoni mwa klabu bora za Ulaya na sasa ni muda wa kwenda mbali iwezekanavyo. Leicester imeshangaza wengi katika michuano lakini mimi binafsi ningependa kukutana ba Barcelona,” Bonucc alisema hayo katika tovuti ya klabu hiyo.
“Kukutana na klabu iliyotunyima fursa ya taji miaka miwili iliyopita litakuwa jambo la maana kubwa kwetu. Baada ya kuishangaza PSG, naweza kusema katika timu zilizobaki Barca wapo katika hali nzuri na wanajiamini.
“Ambaye hatutaki kukutana naye? Bayern Munich. Kila tunapokwenda [Carlo] Ancelotti anajua namna ya kushinda, kama Guardiola. Ni vema kukutana na Bayern kwenye mechi moja tu ya fainali ambapo jambo lolote linaweza kutokea.”
Juve kwa sasa wanaongoza ligi ya Serie A, wakiwa na jumla ya pointi 70 katika mechi 28 ambazo wamecheza.

Comments

Popular posts from this blog

PICHA ZA MUONEKANO WA GARI LA SIMBA SPORT CLUB

Basi la klabu ya Simba SC aina ya Yutong sasa lina muonekano mpya baada ya  wadhamini wazamani TBL kupitia Kilimanjaro kumaliza mkataba wao na timu hiyo. Mwonekano wake safari hii, kuna picha za wachezaji mbalimbali.

MCHEZAJI WA NICE YA UFARANSA AMESEMA ALIKUA MWATHIRIKA WA UBAGUZI WA RANGI

Mchezajiwa wa klabu ya Nice ya nchini Ufaransa Mario Balotelli anasema kuwa alikuwa mwathiriwa wa ubaguzi wa rangi wakati wa mechi ya Ijumaa dhidi ya Bastia. Balotelli ambaye mchezaji hyo wa zamani wa Liverpool mwenye umri wa mika 26 aliandika katika mtandao wa kijamii akisema, ni jambo la kawaida kwamba wafuasi wa Bastia hufanya makelele ya tumbili kwa mechi yote na hakuna mtu katika idara ya adhabu anayechukua hatua? ”Kwa hivyo ubaguzi wa rangi ni sheria halali nchini Ufaransa? Ama ni Bastia pekee? Soka ni mchezo mzuri lakini watu kama wafuasi wa Bastia wanaharibu.Ni aibu kubwa”. Balotelli ambaye alicheza dakika 90 aliporudi uwanjani baada ya kutumikia adhabu yake ya mechi waliyo toka sare ya 1-1 huko Corsica. Ujumbe huo uliotumwa katika mtandao wa Instagram ulisambazwa na Nice katika mtandao wa Twitter wa klabu hiyo. Jopo la adhabu la ligi ya Ufaransa ambalo hutoa maamuzi halijatoa tamko lolote. Balotelli amesha funga mabao 10 katika mechi 15 tangu alivyo jiunga na ...

MARIO BALOTELLI BADO ANDELEZA VITUKO VYAKE

Mchezaji mtukutu Mario Balotelli bado anaendelea na vituko vyake baada ya  kupata kadi nyekundu na kutolewa nje ya dimba kwenye dakika za majeruhi wakati timu yake ya Nice ilipotoka suluhu ya 0-0 na Bordeaux. Hii ilikuwa ni katika mtanange wa Ligi Kuu ya Ufaransa maarufu kama Ligue 1. Sare hiyo ya bila kufungana inaifanya klabu hiyo ya Nice kuzidi kukaribiwa point na klabu ya soka ya Monaco kwenye msimamo wa ligi hiyo ambapo sasa inaongoza kwa tofauti ya alama 2 pekee. Mshambuliaji huyo wa zamani wa Liverpool na Manchester City alipatiwa kadi nyekundu ya moja kwa moja baada ya kumfanyia rafu mbaya Lewczuk ambaye ni beki.