Skip to main content

KOCHA WA ARGENTINA ALICHOKISE KUHUSIANA NA LIONEL MESSI

Moja kati ya vipindi vigumu kwa staa wa soka wa kimataifa wa Argentina anayeichezea FC Barcelona Lionel Messi ni kipindi hiki ambacho Argentina haifanyi vizuri sana, Lionel Messi ambaye ni nahodha wa Argentina aliwahi kulaumiwa na kuandikwa kuwa hajitumi timu ya taifa.
Lionel Messi pia amewahi kutuhumiwa kuwa amekuwa na sauti katika uchaguzi wa wachezaji wa timu ya taifa mbele ya kocha wao Edgardo Bauza madai ambayo kocha Bauza amekuwa akiyapuuzia na kukaa kimya.
lavanguardia_g_874703504-k7ub-u301455491366e5b-992x558lavanguardia-web
Maxi Lopez kushoto akiwa na Lionel Messi wakati wakiwa FC Barcelona
Kocha Bauza ameamua kuzungumzia kuhusiana na maneno hayo “Kwa wale wanaofikiria kuwa Lionel Messi anachagua wachezaji wa kuunda kikosi cha timu ya taifa, sidhani kama kuna haja ya kuwajibu, kama Messi akichagua wachezaji basi nitakuwa nje ya timu”
Kama utakuwa unakumbuka October 14 Lionel Messi alidaiwa kuhusika na kuzuia mchezaji Mauro Icardi asiitwe timu ya taifa, kwa sababu alimchukua mke wa mchezaji mwenzake wa Argentina na rafiki yake ambaye amewahi kucheza nae FC BarcelonaMaxi Lopez.
0012709961

Comments

Popular posts from this blog

PICHA ZA MUONEKANO WA GARI LA SIMBA SPORT CLUB

Basi la klabu ya Simba SC aina ya Yutong sasa lina muonekano mpya baada ya  wadhamini wazamani TBL kupitia Kilimanjaro kumaliza mkataba wao na timu hiyo. Mwonekano wake safari hii, kuna picha za wachezaji mbalimbali.

MCHEZAJI WA NICE YA UFARANSA AMESEMA ALIKUA MWATHIRIKA WA UBAGUZI WA RANGI

Mchezajiwa wa klabu ya Nice ya nchini Ufaransa Mario Balotelli anasema kuwa alikuwa mwathiriwa wa ubaguzi wa rangi wakati wa mechi ya Ijumaa dhidi ya Bastia. Balotelli ambaye mchezaji hyo wa zamani wa Liverpool mwenye umri wa mika 26 aliandika katika mtandao wa kijamii akisema, ni jambo la kawaida kwamba wafuasi wa Bastia hufanya makelele ya tumbili kwa mechi yote na hakuna mtu katika idara ya adhabu anayechukua hatua? ”Kwa hivyo ubaguzi wa rangi ni sheria halali nchini Ufaransa? Ama ni Bastia pekee? Soka ni mchezo mzuri lakini watu kama wafuasi wa Bastia wanaharibu.Ni aibu kubwa”. Balotelli ambaye alicheza dakika 90 aliporudi uwanjani baada ya kutumikia adhabu yake ya mechi waliyo toka sare ya 1-1 huko Corsica. Ujumbe huo uliotumwa katika mtandao wa Instagram ulisambazwa na Nice katika mtandao wa Twitter wa klabu hiyo. Jopo la adhabu la ligi ya Ufaransa ambalo hutoa maamuzi halijatoa tamko lolote. Balotelli amesha funga mabao 10 katika mechi 15 tangu alivyo jiunga na ...

MARIO BALOTELLI BADO ANDELEZA VITUKO VYAKE

Mchezaji mtukutu Mario Balotelli bado anaendelea na vituko vyake baada ya  kupata kadi nyekundu na kutolewa nje ya dimba kwenye dakika za majeruhi wakati timu yake ya Nice ilipotoka suluhu ya 0-0 na Bordeaux. Hii ilikuwa ni katika mtanange wa Ligi Kuu ya Ufaransa maarufu kama Ligue 1. Sare hiyo ya bila kufungana inaifanya klabu hiyo ya Nice kuzidi kukaribiwa point na klabu ya soka ya Monaco kwenye msimamo wa ligi hiyo ambapo sasa inaongoza kwa tofauti ya alama 2 pekee. Mshambuliaji huyo wa zamani wa Liverpool na Manchester City alipatiwa kadi nyekundu ya moja kwa moja baada ya kumfanyia rafu mbaya Lewczuk ambaye ni beki.