Skip to main content

WASANII AMBAO WANATAKIWA KUANGALIA SANA 2017




Billboard ni moja kati ya partners wakubwa sana kwenye muziki duniani, pia wanahusika na upangaji wa chart kubwa zaidi duniani za muziki kupitia mtandao wao, leo ninayo hii kutoka kwao ambapo wameitoa list ya wasanii 10 wanaoanza kufanya vizuri kwenye muziki, jina la star muimbaji Tekno limewekwa kwenye list hiyo.
Wasanii hao ni kutoka sehemu zote duniani na kupitia list hiyo, Tekno ndiye msanii pekee kutoka Afrika aliyetajwa kuwemo kati ya wasanii 10 wa kuwaangalia zaidi mwaka 2017 na wote wanafanya muziki wa Hip-Hop na R&B.
jarida la Billboard pia limethibitisha deal iliyosainiwa kati ya Tekno na kampuni kubwa ya kusambaza muziki duniani “Sony Music” ambapo yeye atakuwa chini studio za Columbia Records.
Billboard wameandika:
“Tekno tayari ana hits kali nchini kwake Nigeria, na Columbia Records wanafahamu hilo, huyu ni msanii mzuri, na ana sauti yenye kuvutia kila mara. Mfano wimbo wake bora zaidi “Pana,” ambao umeshatazama zaidi ya mara milioni 13 kupitia YouTube na wasanii wengine wakaifanyia remix mara nyingi.”
Sio rahisi kumzuia muimbaji huyu kuingia kwenye mainstream kwa jinsi wimbo wake unavyovuta hisia: jaribu kufumba tu macho halafu msimamizi wa vipindi vya radio ambaye yuko smart aukate wimbo wa Drake “Too Good” halafu aipige Pana.” – Billboard
  1. Kehlani
    2. Aminé
    3. YFN Lucci
    4. Leela James
    5. Kodie Shane 
    6. Princess Nokia
    7. Guordan Banks
    8. Tekno
    9. Khalid
    10. H.E.R.
ANGALIA SHOW YA MR BLUE AKIWA MBEYA HAUTAKIWI KUKOSA HIIII

Comments

Popular posts from this blog

PICHA ZA MUONEKANO WA GARI LA SIMBA SPORT CLUB

Basi la klabu ya Simba SC aina ya Yutong sasa lina muonekano mpya baada ya  wadhamini wazamani TBL kupitia Kilimanjaro kumaliza mkataba wao na timu hiyo. Mwonekano wake safari hii, kuna picha za wachezaji mbalimbali.

MCHEZAJI WA NICE YA UFARANSA AMESEMA ALIKUA MWATHIRIKA WA UBAGUZI WA RANGI

Mchezajiwa wa klabu ya Nice ya nchini Ufaransa Mario Balotelli anasema kuwa alikuwa mwathiriwa wa ubaguzi wa rangi wakati wa mechi ya Ijumaa dhidi ya Bastia. Balotelli ambaye mchezaji hyo wa zamani wa Liverpool mwenye umri wa mika 26 aliandika katika mtandao wa kijamii akisema, ni jambo la kawaida kwamba wafuasi wa Bastia hufanya makelele ya tumbili kwa mechi yote na hakuna mtu katika idara ya adhabu anayechukua hatua? ”Kwa hivyo ubaguzi wa rangi ni sheria halali nchini Ufaransa? Ama ni Bastia pekee? Soka ni mchezo mzuri lakini watu kama wafuasi wa Bastia wanaharibu.Ni aibu kubwa”. Balotelli ambaye alicheza dakika 90 aliporudi uwanjani baada ya kutumikia adhabu yake ya mechi waliyo toka sare ya 1-1 huko Corsica. Ujumbe huo uliotumwa katika mtandao wa Instagram ulisambazwa na Nice katika mtandao wa Twitter wa klabu hiyo. Jopo la adhabu la ligi ya Ufaransa ambalo hutoa maamuzi halijatoa tamko lolote. Balotelli amesha funga mabao 10 katika mechi 15 tangu alivyo jiunga na ...

MARIO BALOTELLI BADO ANDELEZA VITUKO VYAKE

Mchezaji mtukutu Mario Balotelli bado anaendelea na vituko vyake baada ya  kupata kadi nyekundu na kutolewa nje ya dimba kwenye dakika za majeruhi wakati timu yake ya Nice ilipotoka suluhu ya 0-0 na Bordeaux. Hii ilikuwa ni katika mtanange wa Ligi Kuu ya Ufaransa maarufu kama Ligue 1. Sare hiyo ya bila kufungana inaifanya klabu hiyo ya Nice kuzidi kukaribiwa point na klabu ya soka ya Monaco kwenye msimamo wa ligi hiyo ambapo sasa inaongoza kwa tofauti ya alama 2 pekee. Mshambuliaji huyo wa zamani wa Liverpool na Manchester City alipatiwa kadi nyekundu ya moja kwa moja baada ya kumfanyia rafu mbaya Lewczuk ambaye ni beki.