Skip to main content

Young Killer aeleza alivyojisikia baada ya Diamond kunukuu mistari minne kwenye nyimbo zake 3 tofauti

Diamond Platnumz ni shabiki mkubwa wa Young Killer.
Na hitmaker huyo wa ‘Marry You’ si mtu anayesikiliza nyimbo za Msodoki juu juu tu, bali kwa undani kiasi cha kushika mistari kadhaa.
Mwishoni mwa wiki, Diamond alionesha wazi kuzimia mistari konde ya rapper huyo wa Mwanza kwa kuandika minne kwenye post zake nne tofauti za Instagram na Twitter.
Mistari ya Young Killer ambayo Diamond ameiandika kwenye post zake za Instagram ni pamoja na:
1. Asa Unataka kuwa mimi na mimi ntakuwa nani….?😩 (Sinaga Swagga (Part1)
2. Naskia Usingizi ni Mbolea ndiomaana tukilala tunaota…?🤔 (Sinaga Swaga Remix)
3. Ukiona Nina changamoto changa Unga tusonge Ugali… Mwisho wa siku wote tunashiba, na Mambo yanakuwa shwari (Sinaga Swagga 1)
4. Shida ingekuwa sumu basi tungekufa wengine (Kumekucha f/ Mr Blue)
“Binafsi nafarijika sababu ni [Diamond] mtu ambaye ana fan base kubwa kwahiyo anapokuwa ameshow love kwa kitu kama hicho kupost mistari yangu hata mashabiki wake pia wanakuwa wananiamini kuwa Young Killer anafanya kazi nzuri,” rapper huyo ameiambia Bongo5.
“Kwahiyo ni moja kati ya msaada, sio lazima akulipie video, akupeleke studio ukarekodi, ni kitu chochote anachoweza kukusaidia kwa namna moja ama nyingine.”
Msikilize zaidi hapo chini:
Audio Player

Comments

Popular posts from this blog

PICHA ZA MUONEKANO WA GARI LA SIMBA SPORT CLUB

Basi la klabu ya Simba SC aina ya Yutong sasa lina muonekano mpya baada ya  wadhamini wazamani TBL kupitia Kilimanjaro kumaliza mkataba wao na timu hiyo. Mwonekano wake safari hii, kuna picha za wachezaji mbalimbali.

MCHEZAJI WA NICE YA UFARANSA AMESEMA ALIKUA MWATHIRIKA WA UBAGUZI WA RANGI

Mchezajiwa wa klabu ya Nice ya nchini Ufaransa Mario Balotelli anasema kuwa alikuwa mwathiriwa wa ubaguzi wa rangi wakati wa mechi ya Ijumaa dhidi ya Bastia. Balotelli ambaye mchezaji hyo wa zamani wa Liverpool mwenye umri wa mika 26 aliandika katika mtandao wa kijamii akisema, ni jambo la kawaida kwamba wafuasi wa Bastia hufanya makelele ya tumbili kwa mechi yote na hakuna mtu katika idara ya adhabu anayechukua hatua? ”Kwa hivyo ubaguzi wa rangi ni sheria halali nchini Ufaransa? Ama ni Bastia pekee? Soka ni mchezo mzuri lakini watu kama wafuasi wa Bastia wanaharibu.Ni aibu kubwa”. Balotelli ambaye alicheza dakika 90 aliporudi uwanjani baada ya kutumikia adhabu yake ya mechi waliyo toka sare ya 1-1 huko Corsica. Ujumbe huo uliotumwa katika mtandao wa Instagram ulisambazwa na Nice katika mtandao wa Twitter wa klabu hiyo. Jopo la adhabu la ligi ya Ufaransa ambalo hutoa maamuzi halijatoa tamko lolote. Balotelli amesha funga mabao 10 katika mechi 15 tangu alivyo jiunga na ...

MARIO BALOTELLI BADO ANDELEZA VITUKO VYAKE

Mchezaji mtukutu Mario Balotelli bado anaendelea na vituko vyake baada ya  kupata kadi nyekundu na kutolewa nje ya dimba kwenye dakika za majeruhi wakati timu yake ya Nice ilipotoka suluhu ya 0-0 na Bordeaux. Hii ilikuwa ni katika mtanange wa Ligi Kuu ya Ufaransa maarufu kama Ligue 1. Sare hiyo ya bila kufungana inaifanya klabu hiyo ya Nice kuzidi kukaribiwa point na klabu ya soka ya Monaco kwenye msimamo wa ligi hiyo ambapo sasa inaongoza kwa tofauti ya alama 2 pekee. Mshambuliaji huyo wa zamani wa Liverpool na Manchester City alipatiwa kadi nyekundu ya moja kwa moja baada ya kumfanyia rafu mbaya Lewczuk ambaye ni beki.