Skip to main content

BAADA YA MAFUA YA NDEGE KUGUNDULIKA NCHI YA UGANDA HAYA NI MAMBO SABA YA KUFUATILIA ILI KUEPUKA

Baada ya ugonjwa wa mafua ya ndege kugundulika nchi jirani ya Uganda baada ya kuwepo kwa vifo vingi vya ndege pori katika maeneo  ya Lutembe beach, Masaka, Kachanga, Bukibanga na Bukakata na vifo hivyo kutokea kwa baadhi ya ndege wafugwao (kuku na bata) na inahisiwa kuwa ndege hao wamepata virusi vya ugonjwa huo kutoka kwa ndege pori wanaohama kutoka nchi za Ulaya.
Baada ya taarifa hizo Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto leo January 18 2017 imetoa taarifa kuhusu kuwepo kwa virusi vya mafua makali ya ndege katika nchi jirani ya Uganda.  Aidha taarifa hiyo imeeleza kuwa maeneo yalioathirika ni maeneo yanayozunguka ziwa Victoria pamoja na ziwa lenyewe.
Taarifa iliyotolewa na wizara ya afya imesema kuwa hadi sasa hakuna binadamu yeyote aliyeonekana kuwa na dalili za ugonjwa huo huko nchini Uganda hivyo wametoa tahadhari  kuwa  kuna uwezekano mkubwa wa ugonjwa kusambaa kwa binadamu ikiwa hatua madhubuti  za kujikinga hazitazingatiwa. 
Taarifa ya wizara imetaja haya ya kuzingatia ili kudhibiti kuenea kwa ugonjwa huo 
  1. Kutoa taarifa endapo wataona kutokea kwa  vifo vya ndege pori au wafugwao (kuku, bata na wengineo) kwa wataalamu wa mifugo, afya au ofisi ya serikali iliyo karibu nawe
  2. Kutokugusa mizoga au ndege wagonjwa bila kutumia vifaa kinga
  3. Kuepukana na tabia ya kuishi nyumba moja  na ndege wafugwao
  4. Kuepuka kuchinja kuku au bata wanaoonyesha dalili yoyote ya ugonjwa 
  5. Kunawa mikono vizuri kwa kutumia sabuni
  6. Kupika nyama au mayai ya ndege kwa muda mrefu usiopungua nusu saa. .
  7. Kuepuka kushika ndege wa porini na ndege wa majumbani wanaohisiwa kuwa na ugonjwa huu.

Comments

Popular posts from this blog

PICHA ZA MUONEKANO WA GARI LA SIMBA SPORT CLUB

Basi la klabu ya Simba SC aina ya Yutong sasa lina muonekano mpya baada ya  wadhamini wazamani TBL kupitia Kilimanjaro kumaliza mkataba wao na timu hiyo. Mwonekano wake safari hii, kuna picha za wachezaji mbalimbali.

MCHEZAJI WA NICE YA UFARANSA AMESEMA ALIKUA MWATHIRIKA WA UBAGUZI WA RANGI

Mchezajiwa wa klabu ya Nice ya nchini Ufaransa Mario Balotelli anasema kuwa alikuwa mwathiriwa wa ubaguzi wa rangi wakati wa mechi ya Ijumaa dhidi ya Bastia. Balotelli ambaye mchezaji hyo wa zamani wa Liverpool mwenye umri wa mika 26 aliandika katika mtandao wa kijamii akisema, ni jambo la kawaida kwamba wafuasi wa Bastia hufanya makelele ya tumbili kwa mechi yote na hakuna mtu katika idara ya adhabu anayechukua hatua? ”Kwa hivyo ubaguzi wa rangi ni sheria halali nchini Ufaransa? Ama ni Bastia pekee? Soka ni mchezo mzuri lakini watu kama wafuasi wa Bastia wanaharibu.Ni aibu kubwa”. Balotelli ambaye alicheza dakika 90 aliporudi uwanjani baada ya kutumikia adhabu yake ya mechi waliyo toka sare ya 1-1 huko Corsica. Ujumbe huo uliotumwa katika mtandao wa Instagram ulisambazwa na Nice katika mtandao wa Twitter wa klabu hiyo. Jopo la adhabu la ligi ya Ufaransa ambalo hutoa maamuzi halijatoa tamko lolote. Balotelli amesha funga mabao 10 katika mechi 15 tangu alivyo jiunga na ...

MARIO BALOTELLI BADO ANDELEZA VITUKO VYAKE

Mchezaji mtukutu Mario Balotelli bado anaendelea na vituko vyake baada ya  kupata kadi nyekundu na kutolewa nje ya dimba kwenye dakika za majeruhi wakati timu yake ya Nice ilipotoka suluhu ya 0-0 na Bordeaux. Hii ilikuwa ni katika mtanange wa Ligi Kuu ya Ufaransa maarufu kama Ligue 1. Sare hiyo ya bila kufungana inaifanya klabu hiyo ya Nice kuzidi kukaribiwa point na klabu ya soka ya Monaco kwenye msimamo wa ligi hiyo ambapo sasa inaongoza kwa tofauti ya alama 2 pekee. Mshambuliaji huyo wa zamani wa Liverpool na Manchester City alipatiwa kadi nyekundu ya moja kwa moja baada ya kumfanyia rafu mbaya Lewczuk ambaye ni beki.